Rekodi yangu haitavunjwa - Mr. Nice

Mr. Nice ameyasema hayo wakati akizungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio na kusema kuwa kwa sasa kazi anazofanya ni kwa ajili tu ya mashabiki wake, ili asiwapoteze lakini hahitaji hata promo.


“Ninachojaribu kukifanya hapa ni kwamba naendelea kuwa mwanamuziki kwa sababu sasa hivi sitafuti promo ya aina yoyote, the only thing I need is respect and money, ni heshima na pesa tu ndio natafuta, , kwa hiyo naendelea kutoa nyimbo nzuri ili niendelee kuwa na mashabiki wangu nisiwapoteze,”, alisema Mr. Nice.

Pamoja na hayo Mr. Nice amesema haitaji kazi zake za sasa zifanye vizuri, kwani hataki kuvunja rekodi aliyoiweka kwenye muziki, kutokana na kazi zake za kwanza.

“Mimi ninachoombea Mungu katika kazi ninazotoa sasa hivi zisibeat rekodi zangu ambazo nimeweka, sababu zitaniharibia rekodi, sitaki kujenga rekodi mpya, rekodi iliyokuwepo ipo kwa sababu haitakaa ivunjwe na hata mwenyewe sitaki kuivunja lakini sio kwa ajili ya kubreak records zangu, rekodi zangu zipo na zitaendelea kuwepo”, alisema Mr. Nice.
Rekodi yangu haitavunjwa - Mr. Nice Rating: 4.5 Diposkan Oleh: Admin